Search This Blog

Friday, July 25, 2014

TOP TEN COUNTRIES WITH THE STRONGEST ARMIES IN AFRICA

Na lssa gombera;  Here is some valid information due to recent estimations and studies. You are welcome to list your own countries if you prefer to believe what comes from your head, but if you are a student or willing to find valid information this will be your first step. 

1. South Africa: South Africa (South Africa has the most powerful army in Africa; it has more harmful weapons than any other country in Africa; it is the only African country that was trying to create the Nuclear weapon but was stopped by the US. The South African National Defence Force (SANDF) this includes: South African Army, South African Navy, South African Air Force and South African Military Health Service. South Africa has recently lower their budge on army from $7.21 billion 2003 to nearly $4 billion 2011. Trained by Israeli, and British, South African solders are more armed and more trained than any other country's soldiers.

 2. Egypt: According to recent study, Egypt is considered to be the second most powerful country in Africa. For many years Egypt has been the first strongest country in the continent of Africa. With number of troops exceed that of South Africa, and more suppliers from countries such as United States, Russia, France, China, Italy and United Kingdom, political instability has made an affect to Egyptian Armed Forces. This includes Egyptian Army, Egyptian Navy, Egyptian Air Force and Egyptian Air Defense Command. Egypt has increased their Armed Forces budget from $3.9 billion to $5.85 billion within the last five years.

 3. Libya:

 4. Morocco:

 5. Nigeria: Nigeria has the second largest army by number of troops, but due to political instability and lack of equipment Nigeria has appear to be the 5th strongest country in Africa. It has been estimated that in year 2013-2018 Nigeria may get weaker. 

 6. Tanzania: Tanzania has the most powerful army in East Africa; The Tanzania Peoples' Defence Force (TPDF) (Swahili: Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) the one defeated Idi Amin of Uganda with big help form Muammar Al-Gaddafi of Libya and . The Palestine Liberation Organization (PLO) The Tanzania People' Defence Force includes Land Forces Command, Naval Command, Air Force Command, and Military Intelligence. Julius Kambarage Nyerere (The first Tanzania's President) prepared president Laurent Desire Kabila of DR Congo to take over the powerful Mobutu Sese Seko Nkuku Ngbendu WA Zabanga; also prepared his son Joseph Kabila. Tanzania has trained Congolese solders in Tabora and Kigoma region for Kabila to return in Congo and take over power. Both Kabilas father and son were schooled and lived most of their lives in Tanzania before returning to Congo. Tanzania Also prepared Yoweri Kaguta Museveni who also schooled and lived in Tanzania before the Tanzania and Uganda war that resulted in defeating Dictator Idi Amin. Most Uganda leader got help from Tanzania before becoming leaders. This includes: Tito Lutwa Okello, Yusuf Kironde Lule, and Bazilio Olara-Okello. Recently, Tanzania did not want to send his solders in Somalia but offer training to Somali solders who will soon return to protect their country. Tanzania sent 924 soldiers to lead the African Union Solders in Comoros's Island to take Colonel Mohamed Bacar of Anjouan off power. Tanzania has the 3rd largest army in number troops after Ethiopia, and Eritrea, and recently considered the second in equipment after Kenya, but with more well trained troops. The recent estimation shows that Tanzania is the country in East-Africa followed by Ethiopia. 

7. Ethiopia: Ethiopia once was considered the strongest country in East Africa. After continues civil war Ethiopia has gotten weaker. Ethiopia is still has the largest army by number of troops followed by Eritrea and Tanzania, and the 3rd in equipment after Kenya and Tanzania. 2011 Estimation shows, Ethiopia is spending 2.4% of its GDP in military. This includes: Ethiopia Army and Ethiopia Air Force. 

 8. Ghana: 

 9. Kenya: Kenya is the second strongest Nation in East Africa Economically after Ethiopia; it is the first in East African Community followed by Tanzania and Uganda. In 1981 Kenya was consider to be the 4th strongest nation in East Africa after Tanzania, Ethiopia, and Somalia. In 1994 Kenya was considered the 3rd strongest country in East Africa after Somalia and Uganda having both economic and political instability caused by war and dictatorship. The estimation indicates that Kenya will get even stronger within next 5-10 years. Kenya has the higher army budget in East Africa followed by Ethiopia. 2012 estimation shows Kenya is using 5.3% of its GDP in military. This includes: Kenya Army, Kenya Navy and Kenya Air Force. 

10. Uganda

Sunday, July 7, 2013

HII NDIO HABARI INAYOTIKISA ULIMWENGU MUDA HUU,NDEGE KUBWA YATUA GHAFLA NA KUWAKA MOTO


A fire truck sprays water on Asiana Flight 214 after its crashed at san Fransisco International Airport on saturday 6 Juky 2013, in San Fransisco.Photo By AP/BERGER

SAN FRANCISCO (AP) — An Asiana Airlines flight from Seoul, South Korea, crashed while landing at San Francisco International Airport on Saturday, forcing passengers to jump down the emergency inflatable slides to safety. It was not immediately known whether there were any injuries.


The Boeing 777 was supposed to land on runway 28 left at the airport, said Federal Aviation Administration spokeswoman Laura Brown. She said the sequence of events was still unclear, but it appeared the plane landed and then crashed.

A video clip posted to YouTube shows smoke coming from a silver-colored jet on the tarmac. Passengers could be seen jumping down the inflatable emergency slides. Television footage showed debris strewn about the tarmac and pieces of the plane lying on the runway. Fire trucks had sprayed a white fire retardant on the wreckage. A call to the airline seeking comment wasn't immediately returned.

Asiana is a South Korean airline, second in size to national carrier Korean Air. It has recently tried to expand its presence in the United States, and joined the oneWorld alliance, anchored by American Airlines and British Airways.

The 777-200 is a long-range plane from Boeing. The twin-engine aircraft is one of the world's most popular long-distance planes, often used for flights of 12 hours or more, from one continent to another. The airline's website says its 777s can carry between 246 to 300 passengers. The last time a large U.S. airline lost a plane in a fatal crash was an American Airlines Airbus A300 taking off from JFK in 2001.

Smaller airlines have had crashes since then. The last fatal U.S. crash was a Continental Express flight operated by Colgan Air, which crashed into a house near Buffalo, N.Y. on Feb. 12, 2009. The crash killed all 49 people on board and one man in a house.

CHUKUA NAFASI YAKO KUJUA MARRAPA WENYE FEDHA NYINGI ZAIDI MWAKA 2013 DUNIANI



diddy
The Richest Rappers In The World 2013:
  • 1. Diddy – Net Worth: $580 million (up $80 million)
  • 2. Jay-Z – Net Worth: $500 million (up $25 million)
  • 3. Dr. Dre – Net Worth: $360 million (up $100 million)
  • 4. Master P – Net Worth: $350 million (no change)
  • 5. 50 Cent – Net Worth: $260 million (up $10 million)
  • 6. Birdman – Net Worth: $150 million (up $35 million)
  • 7. Eminem – Net Worth: $140 million (up $20 million)
  • 8. Snoop Dogg – Net Worth: $130 million (up $10 million)
  • 9. Ice Cube – Net Worth: $120 million (up $20 million)
  • 10. Lil Wayne – Net Worth: $110 million (up $15 million)
  • 11. Kanye West – Net Worth: $100 million (up $10 million)
  • 12. LL Cool J – Net Worth: $85 million (up $5 million)
  • 13. Timbaland – Net Worth: $80 million (up $5 million)
  • 14. Pharrell Williams – Net Worth: $80 million (up $2.5 million)
  • 15. Akon – Net Worth: $80 million (up $2.5 million)
  • 16. Beastie Boys - $75 million each (no change)
  • 17. Ludacris – Net Worth: $75 million (up $5 million)
  • 18. Busta Rhymes – Net Worth: $65 million (up $5 million)
  • 19. Nelly – Net Worth: $60 million (no change)
  • 20. T.I. – Net Worth: $40 million (up $10 million)
  • 21. Big Boi – Net Worth: $40 million (no change)
  • 22. T-Pain – Net Worth: $35 million (up $5 million)
  • 23. Ice-T – Net Worth: $35 million (up $5 million)
  • 24. Drake – Net Worth: $30 million (up $5 million)
  • 25. Rick Ross – Net Worth: $28 million (up $3 million)
  • 26. Nicki Minaj – Net Worth $25 million (up $5 million)
Source: Celebrity Net worth Inc

Thursday, June 27, 2013

UJIO WA OBAMA KUFURU


Na Issa Gombera
Na Mwandishi Wetu
UJIO wa Rais wa Marekani, Barack Obama ni kufuru tupu, kiasi cha fedha ambacho kinachotumika kugharamia ziara yake peke yake kinazidi mara mbili ya kile kilichoteketea pale mtangulizi wake, George W. Bush, alipotembelea nchini mwaka 2008.
Rais wa Marekani, Barack Obama.
Obama, rais wa kwanza mwenye asili ya Bara la Afrika kutawala Marekani, atawasili nchini Julai Mosi, mwaka huu na kufanya ziara ya siku mbili.
Inaaminika kuwa Bush alipokuja nchini, msafara wake uliigharimu Marekani kiasi cha dola milioni 50 (shilingi bilioni 80) lakini Obama na timu yake watatumia mara mbili ya hapo, yaani dola milioni 100 (shilingi bilioni 160).
Hesabu hiyo, ilimtisha hata Mbunge wa Singida Mjini (CCM), Mohamed Dewji ‘Mo’ ambaye aliandika kwa mshangao katika akaunti yake ya Twitter, Jumamosi iliyopita: “Ujio wa Obama Tanzania utaigharimu Marekani dola milioni 100.”
UKUBWA WA MSAFARA
Kwa mujibu wa ziara mbalimbali ambazo Obama alishazifanya tangu alipoingia madarakani Januari 2009, msafara wake huwa na watu zaidi ya 800.
Obama ambaye ni Rais wa 44 wa Marekani, akiwa na mkewe, Michelle, huongozana na watu 500 ambao ni watumishi wa kawaida wa Ikulu ya Marekani, White House.
Katika wahudumu hao 500, wapo madaktari sita pamoja na wauguzi wengine zaidi ya 30, wapishi na kadhalika.
Msafara wa Obama, haukamiliki bila walinzi karibu 300 ambao jukumu lao huwa ni kumlinda rais huyo kwa ukaribu zaidi.
Kutokana na hesabu hiyo ni wazi kuwa Tanzania itakuwa na msukosuko wa aina yake pale Obama atakapowasili Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Hata hivyo, kwa vile ndege ya Rais wa Marekani, Air Force One, haina uwezo wa kubeba idadi hiyo ya watu, wengi wao watawasili kwa mafungu wiki hii ili kufanya maandalizi ya ujio wake.
Ulinzi wa Obama.
MASHUSHUSHU KILA KONA
Kuelekea siku ya ujio wa Obama, Jiji la Dar es Salaam, limeshawekwa chini ya ulinzi, mashushushu kutoka Marekani wametanda kila kona kuhakikisha rais huyo hapatwi na zahama yoyote akiwa nchini.
Maofisa wa CIA (Central Intelligence Agency) ambao kiuhalisia ndiyo Idara ya Usalama wa Taifa la Marekani, wanadaiwa kuwepo nchini tangu Januari, mwaka huu, lengo likiwa ni kuratibu na kuhakiki usalama wa nchi.
Vilevile inadaiwa, makomandoo wapatao 400 kutoka Taasisi ya Upelelezi ya Marekani, FBI (Federal Bureau of Investigation), waliwasili nchini kwa mafungu kuanzia mwishoni mwa mwaka jana, jukumu lao likiwa ni kuweka mambo sawa.
Madai hayo yanajengwa na hoja kwamba hata pale FBI walipojitolea kutoa mchoro wa mtu aliyedaiwa kumpiga risasi na kumuua Padri Evarist Mushi, Machi mwaka huu, ilikuwa ni kwa haraka sana.
“Wale FBI walikuwa hapahapa Tanzania ndiyo maana walijitolea kutoa mchoro wa Padri Mushi kwa haraka sana, ingekuwa wapo Marekani wasigejitolea haraka vile.
“Sema sasa ilikuwa siri kubwa. Taarifa za ujio wa Obama kuja zipo tangu mwaka jana ila zilifanywa siri kwa sababu za kiusalama,” alisema ofisa mmoja wa Ikulu ya Tanzania kwa sharti la kutotajwa jina lake gazetini.
Gari la Obama.
ANAKUJA NA MAGARI 21
Kwa mujibu wa taarifa za ziara za Rais  Obama, kiongozi huyo husafiri na jumla ya magari 21.
Obama husafiri na gari lake binafsi kama Rais wa Marekani aina Limousine Cadillac, ambalo halilipuki wala kuharibika hata likipigwa na bomu.
Gari hilo likilipuliwa na bomu, matairi peke yake ndiyo huungua lakini hubaki na rimu ambazo hutembea kwa umbali wa kilometa 500 bila wasiwasi.
Limousine Cadillac ambalo ni toleo maalum la mwaka 2009 kwa ajili ya Obama pekee, huambatana na magari mengine 20.
Kutokana na tafsiri hiyo, Obama akiwa nchini, atakuwa na msafara wake uliokamilika na unaojitegemea kwa asilimia 100.

MAGARI 21 YATAKUJA VIPI?
Habari zinasema kuwa Limousine Cadillac ndilo litakalokuja na Air Force One, Julai Mosi, mwaka huu, mengine 20 yatawasili kabla ya ujio wa Obama.
Inaelezwa kuwa sababu ya magari hayo 20 kutokea Marekani ni kwamba utaratibu wa White House unaeleza kuwa msafara wa Rais wa Marekani ndani ya nchi unapaswa kufanana na wowote ule anapokuwa nje ya nchi.
Habari zinaeleza kuwa magari hayo 20, yatawasili na manowari kubwa ya Marekani ambayo inategemea kuwasili nchini wakati wowote kupitia Bahari ya Hindi.
Inaelezwa kuwa kazi nyingine ya manowari hiyo ni kudumisha usalama baharini, kuhakikisha watu wenye lengo la kufanya uvamizi hawafanikiwi kwa njia ya majini katika kipindi hiki cha siku chache kabla ya ujio wa Obama na hata pale akiwepo.

HOTELI ZA NYOTA TANO ZAJAA
Uchunguzi wa Risasi Mchanganyiko  umebaini kuwa ujio wa Obama umekuwa na neema kwa hoteli zenye hadhi ya nyota tano ambazo karibu zote zimekodiwa jumla.
Hoteli hizo zimechukuliwa na Marekani kwa ajili ya watu watakaombatana na Obama ikiwemo wahudumu pamoja na walinzi mbalimbali.
Inaelezwa, baadhi ya hoteli kuna wateja walihamishwa wiki mbili kabla ili kupisha wageni kutoka Marekani ambao wamekuwa wakiwasili nchini kwa mafungu.

WENYE MAGARI MAPYA WAULA
Uchunguzi zaidi umebaini kuwa wamiliki wa magari mapya yenye nafasi, hususan Toyota Noah, kwao ni neema ya aina yake.
Risasi Mchanganyiko limebaini kuwa wenye magari hayo hutakiwa kuripoti Ubalozi wa Marekani nchini kisha vyombo vyao hupimwa kuona uzima wake.
Habari zinasema, kila mwenye gari ambalo litafuzu vipimo, atalipwa shilingi 200,000 kwa siku katika kipindi chote litakapotumika katika ziara hiyo ya Obama.

BUSH NAYE ANAKUJA
Katika hatua nyingine, Bush ambaye ni Rais wa 43 wa Marekani, atawasili nchini hivi karibuni.
Hii ina maana kuwa kipindi ambacho Obama atakuwepo nchini, Bush naye atakuwepo ndani ya Tanzania.
Bush yeye anakuja kwa ajili ya kuhutubia mkutano wa wake za marais mbalimbali duniani ambapo imeelezwa kuwa mke wa Obama, Michelle, naye atahudhuria.

 KARIBU OBAMA
Ujio wa Obama ni fahari ya Tanzania kwamba nchi yetu ni salama na inavutia ndiyo maana hata kiongozi huyo wa taifa kubwa kabisa duniani, ameweza kushawishika kuja.
Karibu sana Tanzania Rais Obama. MHARIRI.

OBAMA ASIFU SENEGAL KWA DEMOKRASIA

 27 Juni, 2013 - Saa 13:46 GMT
Obama anatarajiwa kwenda Afrika Kusini kisha Tanzania kwa ziara yake ya pili Afrika
Rais wa Marekani Barack Obama ambaye yuko katika ziara yake ya Afrika, amesifu nchi ya Senegal kwa kuwa moja ya nchi zenye demokrasia thabiti barani Afrika.
Akiwahutubia waandishi wa habari nchini Senegal kwa mkondo wake wa kwanza wa ziara yake Afrika,baada ya mazungumzo na rais Macky Sall, Bwana Obama alisema kuwa Senegal iliandaa uchaguzi huru na wa haki pamoja na kuwa na kipindi salama cha mpito.
Pia aliisifu kwa kuwa na mtindo wa kusuluhisha migogoro kwa mazungumzo na mashauriano, wala sio kwa njia ya ghasia.
Alisema kuwa Afrika kama bara limepiga hatua kubwa upande wa demokrasia katika miaka ya hivi karibuni.
Obama atazuru Afrika Kusini ambako rais mstaafu Nelson Mandela anaugua sana na amelazwa hospitalini.
Aliwaambia waandishi wa habari kuwa wanamuombea Mandela pamoja na familia yake.

Sunday, June 23, 2013

UJIO WA RAIS OBAMA TANZANIA WAWATESA MACHINGA NA WAUZA MAGAZETI POSTA

 Na. Issa Gombera

Rais Barack Obama wa Marekani  akisalimiana na Rais  Jakaya  Kikwete alipotembelea nchini Marekani hivi karibuni
Rais Obama
Hali  ilivyo kwa  sasa  eneo la Posta  mpya  jijini Dar es Salaam baada ya wafanyabiashara  ndogo ndogo machinga  na  wauza magazeti na vocha  eneo  hilo  kuondolewa na mgambo  wa  jiji katika zoezi la kusafisha jiji kwa ajili ya ugeni  huo mkubwa nchini

.....................................................

ZIKIWA zimebaki  siku chache kabla  ya  Rais  wa Marekani Barack Obama  kufanya  ziara  yake chini Tanzania ,wafanyabiashara  ndogo ndogo maarufu kama Machinga na  wauza magazeti na  vocha eneo la Posta mpya  jijini Dar es Salaam  wamedai  kunyanyasika na mgambo  wa  jiji kupitia msako mkali unaofanyika .
Msako  huo  umeanza mapema asubuhi ya  leo katika  eneo hilo la Posta na maeneo mbali mbali ya jiji la Dar es Salaam ambako msafara wa Rais Obama utapita kutokea  uwanja  wa kimataifa  wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere kuelekea Ikulu ya Dar es Salaam 

Wakizungumza na mtandao  huu wa www.matukiodaima.com baadhi ya  wafanyabiashara  hao ambao wamelazimika  kusitisha shughuli za biashara  zao  eneo  hilo ,wamesema  kuwa mbali ya ujio  huo  wa Rais Obama nchini  kuwa ni heri kwa Taifa  ila kwa upande  wao wanapinga hatua ya mgambo  kuwanyanyasa kwa  kuwatimua  eneo hilo ambalo  siku  zote  wamekuwa wakifanya kazi na mbaya  zaidi  wameamua kuwatimua hadi  wauza magazeti .

 Alisema mfanyabiashara  Ally Husein  kuwa  kutokana na siku ya  ziara ya Rais Obama  kuwa bado kama  takribani siku 12 mbele  ni  vema uongozi  wa jiji na mkoa  wa Dar es Salaam ukatumia busara  zaidi kwa  kuwaacha kwa  siku hata 7 mbele ama tano  ili  waendelee na biashara kwa ajili ya  kujitafutia mahitaji yao ya  kila  siku kuliko kuwazuia kuanzia leo .

"Kweli  ujio  huu  wa Rais Obama  unatutesa  sana  sisi  walalahoi ambao tunategemea  kuendesha maisha  yetu kwa kuwepo hapa Posta kwa kufanyabiashara za kuuza magazeti na vocha.....Serikali ya mkoa  wa Dar es Salaam tunaomba ilitazame kwa undani  zaidi suala  hili la kutulaza njaa kwa siku zote 12 bila kufanya shughuli"

Hata  hivyo alisema  kuwa  idadi kubwa ya  wafanyabiashara  eneo hilo wamekuwa wakiendesha biashara  zao kwa kupitia mikopo hivyo kuzuiwa kwa muda  wote  huo kutawaharibia mwelekeo  wa kimaisha  .

Hivyo  alishauri  serikali kuwa katika maandalizi ya  ujio  wa Rais  Obama nchini  bado  kutumia njia nzuri ya  kuweka  jiji  safi pasipo kuwaumiza  wananchi  wenye  kipato cha chini wanaofanya  shughuli zao katika eneo hilo.

"Hivi kama  siku  zote  tumekuwa  tukiuza magazeti katika eneo hilo na hakukuwa na uchafuzi  wowote wa mazingira  leo serikali inatuondoa eneo hili na kutuona kama ni uchafu ....kweli katika  hili ni  kutunyanyasa  wanyonge

Monday, June 17, 2013

KIFO CHA MANGWEA MAPYA YAIBUKA

KIFO CHA NGWEA... MAPYA YAIBUKA!

Na Waandishi Wetu
HUKU mwili wake ukitarajiwa kuwasili Bongo kesho, kifo chake Albert Mangweha ‘Ngwea’ kilichotokea katika hali ya utata Mei 28, 2013 nchini Afrika Kusini, kimeibua mambo mapya, Ijumaa Wikienda lina mzigo wote.
Picha ya Mangweha iliyowekwa kwa ajili ya waombolezaji.
MAMA MANGWEA NAYE AZIDIWA, AKIMBIZWA HOSPITALI YA MKOA 
Habari kutoka msibani Moro jana zilisema mama mzazi wa marehemu Mangwea, Denisia Mangwea naye alizidiwa na kukimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu zaidi.
Kwa mujibu wa baadhi ya waombolezaji msibani hapo, mama huyo alipata mshtuko wa moyo kufuatia kifo cha mwanaye ambapo taarifa za kifo hicho zilimshtua tangu Jumanne mpaka alipozidiwa jana. 
Msanii M to the P akiwa hospitalini. (Picha kwa hisani ya Clouds FM.)
HABARI KUTOKA SAUZI SASA
Habari kutoka kwenye Jiji la Johannesburg ambako Ngwea alifia, mtiririko wa maelezo ya wenyeji wa Mangwea na Mgaza Pembe ‘M 2 The P’ nayo yanaibua mapya ambayo awali yalikuwa hayajulikani. 

MAELEZO YA SAUTI ZA WENYEJI
Wakizungumza hewani kupitia redio moja ya jijini Dar, wenyeji wao wawili waliojitambulisha kwa jina moja moja la Godfrey na Godluck ambao walikuwa na Mangwea na M 2 The P, kila mmoja alisema lake huku maelezo yao yakionesha dalili ya kutofautiana au kuzua maswali masikioni mwa watu.
Mama mzazi wa Mangwea, Denisia Mangwea.
KUMBE WALITOKA KLABU SALAMA
Godluck siku hiyo aliwaendesha wawili hao kutoka klabu kurudi nyumbani walikofikia kwa wiki mbili nyuma ambako ni kwa Godfrey. Godluck alikuwa akitumia gari lake.
Kwa mujibu wa Godluck, waliondoka klabu alfajiri kurudi nyumbani kwa Godfrey au God wakiwa salama salimini. Waligonga mlango, God akatoka kufungua, wakaigia ndani wote.
Godluck anaishi sehemu tofauti na nyumba hiyo, lakini kwa sababu saa 2:00 asubuhi Ngwea na M 2 The P walitakiwa kurejea Bongo na ni yeye ndiye aliyetakiwa kuwapeleka uwanja wa ndege, hivyo aliamua kulala palepale.
Alisema wakiwa chumbani, watu wanne, yeye, Ngwea, M 2 The P na mwenyeji Godfery, Ngwea alianza kuonesha dalili za kushangaza.
Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Radhia Msuya (katikati) akibadilishana mawazo na baba mdogo wa marehemu David Mangweha (kulia) na mama mdogo Ella (kushoto).
“Kule chumbani Ngwea alikuwa ananilalialalia huku amelegea, nikawa namuuliza we vipi? Hanijibu, mara akanitapikia, nikamwamsha hakuamka, nikamwamsha God (Godfrey) na kuuliza huyu vipi? Nikamwamsha M 2 The P, nikamuuliza huyu vipi, mbona ananitapikia, akasema huyo ndiyo zake akilewa huwa anakuwa hivyo, si unajua mambo yake tena,” alisema Godluck akikariri maneno ya M 2 The P.
Aliendelea kusema kuwa ghafla alimuona M 2 The P naye kama akaanza kuzidiwa. “Nikamuuliza we vipi? Lakini nikajua labda ni haya mambo yao, maana unajua mimi nilikuwa siwaelewielewi,” alisema Godluck.
Alisema ilipofika saa mbili asubuhi, akiwa anajua wasafiri hao wameshachelewa ndege, yeye aliamua kuondoka kurudi kwake ambako si mbali akipanga kwenda kulala hadi mchana.
Akasema: Lakini nikiwa nakwenda nyumbani, NILIMPIGIA SIMU MIDO, dogo mmoja anaishi jirani, nikamwambia wale jamaa (akina Ngwea) kama wamezidiwa, nenda kawacheki.
Alisema akiwa amelala, aliamshwa na simu ya Mido, akaipokea na kuambiwa hali za jamaa hao ni mbaya sana hivyo yeye akalazimika kwenda na kuwapakia kwenye gari lake WOTE WAWILI hadi Hospitali ya St. Hellen Joseph  ambako ilithibitishwa na daktari kwamba, Ngwea aliaga dunia ila M 2 The P hali  tete.

MAELEZO YA GODFREY SASA
“Siku ya mwisho, walitoka wakarudi asubuhi, wakanigongea mlango, nikawafungulia. Wakaingia, Ngwea akaniambia NICHUKUE ‘KONTAKTI’ (mawasiliano) yake, nikachukua notebook yangu na kuandika. Walikuwa wazima kabisa.
“Basi, tukawa tunaongeaongea pale kama mtu wa kawaida tu. Hakuniambia kama anaumwa popote wala hakula chochote.
“Baadaye ndiyo wote wawili wakazidiwa, tukawachukua kuwapeleka hospitali ambako daktari alisema Ngwea alifariki dunia lakini M 2 The P hali yake ilikuwa mbaya akalazwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi (ICU).”

KUNA MADAI MAITI YA
NGWEA ILITUPWA NJE YA JIJI
Mtangazaji alimuuliza Godfrey kuhusu madai kwamba, kabla ya Ngwea kupelekwa hospitalini, mwili wake ulikutwa nje ya Jiji la Johannesburg ukiwa umetupwa.
Godfrey: Si kweli, alizidiwa palepale nyumbani ndiyo tukamchukua kumpeleka hosptali. NGWEA NILIMPAKIZA KWENYE GARI LANGU, mwenzake alikuwa kwenye gari la nyuma. 

MASWALI MAGUMU
Katika maelezo ya wawili hao, Godluck alisema alipokuwa anarudi kwake, alimpigia simu dogo anaitwa Mido na kumwambia kuhusu kuzidiwa kwa akina Ngwea aende akawacheki, kwa nini asimpigie simu Godfrey ambaye ndiye mwenyeji wa wawili hao, ndiye aliyewafungulia mlango na ndiye aliyemwamsha  kumwambia kuhusu hali ya Ngwea?
Godluck yeye alisema aliwapakia wawili hao kwenye gari lake hadi hospitali, lakini Godfrey alisema alimpakia Ngwea kwenye gari lake na M 2 The P alipakiwa kwenye gari jingine la nyuma yake (labda la Godluck).
Godfrey, kwa mtangazaji alikiri kuishi na Ngwea kwa wiki mbili, lakini pia akasema usiku wa kuamkia kifo chake marehemu alimpa mawasiliano, ina maana hakuwa na kontakti za Ngwea kwa siku zote kumi na nne alizoishi pale?

MANENO YA MAMA YAKE MZAZI
Jumamosi iliyopita, mwandishi wetu mkoani Morogoro alifika msibani na kufanikiwa kukutana na mama mzazi wa Ngwea, Denisia Mangwea akiwa na majonzi mazito ambapo alisema:
“Mwanangu Albert amekwenda, najua sitamuona tena katika maisha ya duniani, inaniuma sana. Nilimpenda sana na yeye alinipenda sana lakini Mungu kaamua kumchukua.”

MAZIKO
Kumekuwa na utata wa kuwasili kwa mwili wa marehemu Ngwea, awali ilidaiwa ungefika jana na kuzikwa Jumanne, Kihonda Morogoro, lakini baadaye ikadaiwa mwili huo sasa utawasili kesho Jumanne.
Wakati hayo yakiendelea, jana Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Radhia Msuya alikwenda nyumbani kwa baba mdogo wa marehemu Ngwea, David Mangwea, Mbezi Beach, Dar na kusaini kitabu cha maombolezo.
MUNGU ailaze pema peponi roho ya marehemu Mangweha. Amina.